Advertisement

Breaking

Monday, September 26, 2016

Watafiti wabaini faida hii ya ajabu kwa wanaume wanaoshiriki tendo la ndoa mara nyingi

Watafiti wa Kizungu wanakesha kufanya tafiti chungu mzima na zingine majibu yake zinaweza kukuacha mdomo wazi.

Kwa mfano huu – jamaa eti wamebaini kuwa kushiriki tendo la ndoa mara nyingi kunaongeza imani ya kiroho na hata imani kwa Mungu! Makubwa..

Kwa mujibu wa utafiti, tendo la ndoa hutoa homoni ya upendo iitwayo oxytocin ambayo haiishi tu kutengeneza ukaribu wa kijamii bali pia imani ya Mungu – hususan kwa wanaume.

Watafiti katika chuo kikuu cha Duke cha North Carolina, wanasema kuwa tendo hilo huhamasisha imani – ama kuongeza imani katika Mungu na dini.

Utafiti huo umeliochapishwa mwishoni mwa wiki unaangalia homoni ya oxytocin ambayo huamshwa zaidi wakati wa kufanya mapenzi, wakati wa kuzaa na wakati wa kunyonyesha.

No comments:

Post a Comment

Sponsor