Advertisement

Breaking

Thursday, October 6, 2016

Mrembo Amber Lulu Adaiwa Kukamatwa na Madawa ya Kulevya..Marafiki zake Wamkana Live

Mwanadada mrembo ambae amejipatia umaarufu mkubwa siku za karibuni kwa kutokea katika videos kadhaa za Bongo Fleva Amber Lulu inasemekana kwamba yuko chini ya usimamizi wa polisi kwa siku ya pili sasa.
Sababu ya kuwa chini ya Ulinzi inasemekana kuwa amekamatwa na Sembe (Madawa ya kulevya) huko Airport mkoani Arusha akijiandaa kuyasafirisha hadi nchini China.Gossip Cop Soudy brown alizinyaka taarifa hizo na akaona haitakuwa mbaya kama atapiga story na watu wa karibu wa mwanadada Amber Lulu ili kupata ukweli juu ya suala hilo.Ndipo alipomvutia waya Gigy Money. Mapovu yaliyomtoka mwanadada Gigy sio ya polepole, na kudai kuwa kimbelembele cha mwanadada Amber Lulu ndio kimemfanya kupata matatizo.
Soudy Brown hakuishia kwa Gigy tu, alimvutia waya na rapper Young Deeambaye kwa mujibu wa Gigy Money inasemekana kuwa ndiye boyfriend wa mwanadada Amber Lulu. Na Young Dee alikana kabisa kumjua mrembo huyo na akadai kuwa hajui chochote kinachoendelea kuhusiana na msichana huyo.
Ubuyu wote nimeukusanya hapa chini kwenye hii video unaweza kuitazama.

No comments:

Post a Comment

Sponsor