Advertisement

Breaking

Wednesday, October 5, 2016

Wi-Fi kupatikana bure maeneo ya umma na burudani Dar

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amezindua mpango wa kuweka huduma ya mtandao wa Wi-Fi katika maeneo ya umma na yale ya burudani jijini Dar es Salaam.

Utekelezaji wa mradi huo wa kampuni ya mawasiliano nchini, utapanua huduma za mawasiliano ili kuweza kuwafikia watu wengi zaidi na hivyo kuimarisha uchumi.

“Tunawapongeza kwa kutekeleza mradi huu na tunatumai upandaji wa miti katika maeneo tofauti mjini ikiwemo maeneo ya burudani, watu wataweza kupata huduma ya mtandao,” alisema Bi Samia.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amesema kuwa mradi huo juhudi za serikali ya awamu ya tano, kuimarisha huduma kadhaa hususan mawasiliano na huduma za mtandao kwa wote.

No comments:

Post a Comment

Sponsor