Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
“Asante sana Fred”
Wakiwa
juu angani, wakaendelea kupata vinywaji mbalimbali, huku wakitazama
baadhi ya chanel, za tv ndogo iliyopo kwenye kila meza ya safa lililopo
ndani ya ndege hiyo ya kifahari. Gafla Rahab akaanza kujihisi vaibaya
vibaya, huku mara kadhaa, akawa anajikaza ili Praygod asijue ni kitu
gani kinacho endelea, ila gafla akajikuta akianza kutapika na kulichafua
gauni lake alilo livaa
ENDELEA
Furaha
ikabadilika na kuwa mshike mshike ndani ya ndege kwani kadri muda
ulivyo zidi kwenda hali ya Rahab ikaanza kubadilika na kujikuta mwili
mzima ukianza kumtetemeka, na kutoa mapuvu mdomoni mwake. Frednando
akawaamuru marubani wairudishe ndege haraka kwenye kiwanja cha nyumba
kwake ili kumuwahisha Rahab, aweze kuonana na madktari.
Macho
ya Rahab yakabadilika na mboni zake nyeusi zikapotea na kubaki weupe
kwenye macho yake jambo lililozidi kumchanganya raisi Praygod pamoja na
Frednando ambaye hakujua ni ugonjwa gani ambao bibi harusi ameweza
kuupata.
Haikuchukua
muda mwingi, matairi ya ndege yakawa yanaserereka kwenye ardhi ya
uwanja wa nyumbani kwa Frednando, ambapo Alisha waeleza madaktari wake
wawe tayari kwa kumpokea mgonjwa.
Kwa
kushirikia na Frednando, wakambeba Rahab na kumtoa nje ya ndege na
kumuingiza kwenye gari maalumu la wagonjwa lililokuwa likiwasubiri. Moja
kwa moja Rahab akakimbizwa kwenye jingo linalo tumiwa na Fredando kama
hospitali inayo mtibu yeye na familia yake pale wanapo patwa, na hali
yoyote ya kuumwa. Uzuri wa eneo lilipo jumba la Frednando, aliweza
kuwekeza pesa nyingi kujijengea vitu muhimu kwa mahitaji yake, ikiwemo
jengo la hospitali, lenye madaktari bingwa ambao Fredinando anawaamini
sana
“Kaka hivi mke wangu atapona kweli?”
Raisi
Praygod alizungumza huku machozi yakimlenga lenga, akamshuhudia mke
wake akipakizwa kwenye kitanda cha matairi baada ya kushushwa ndani ya
gari, na moja kwa moja akaingizwa kwenye chumba kilicho jaa vifaa muhimu
kwa kumuhudumia mgonjwa mahututi
“Atapona tu, usijali rafiki yangu”
Fredinando
alimfariji raisi Praygod, lakini yeye mwenye amechanganyikiwa kwani
hakuamini kama siku kama hiyo kutajitokeza jambo kama hilo la
kuhuzunisha. Wakiwa wamesimama kwenye nje ya mlango wenye kioo kikubwa,
wakawashuhudia madaktari wakitumia mashine za kustulia mapigo ya moyo
wakiziweka kwenye kifua cha rahabu ambaye amezima kabisa mapigo yake ya
moyo.
Machozi taratibu yakaanza kumtoka raisi Praygod, hakuamini uzuri wote wa Rahab, unaweza kupotea muda wowote kuanzia sasa.
“Kaka jikaze”
Frednando
alizungumza huku, naye machozi yakiwa yanamtiririka, uchungu anao upata
rafiki yake, nao unaugusa moyo wake, kwani ni dakika chacha tu wametoka
kucheka na kufurahi na shemeji yake ambaye muda mwingi anapenda
kumtania kwa jina la ‘AFRICAN QUEEN’. Mashine zakupulia zinazo soma
mapigo ya moyo jinsi yanavyo kwenda yakazidi kuwachanganya madaktari
hawa wane, kwani ni mstari mmoja ulio nyooka ndio unakatiza kwenye
mashine hiyo, huku kukisomeka sifuri mbili za rangi nyekundu zikiashiria
kwamba Rahab mapigi ya moyo hayafanyi kazi, moja inawezekana amesha
fariki au moyo wake upepata mstuko mkubwa
***
Si
Fetty wala mwenzake yoyote aliye weza kujinyanyua kutoka kwenye sakafu
walipo kaa, kila mmoja macho yake yaliyo jaa machozi, wakawa wanaitazama
sura ya kipande cha mwanaume, aliye fura kwa hasira na si mwingine bali
ni bwana Rusev, aliye simama huku bastola yake ikiwa mkononi mwake.
Kila mmoja akatamani kujitetea, ila nguvu hakuwa nazo za kutosha kusema
anaweza kupambana na bwana Rusev, anaye onekana kuchukia baada ya
mapiganaji yake matatu kuuliwa kinyama
“Hatuna tulicho kibakisha tena duniani, tumekuwa ni watu waovu. Hatuna pa kwenda zaidi ya kaburini. Tuue sisi yupo tayari”
Anna
alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, huku mikono yake
yenye kufungwa pingu akiendelea kumshika Halima, aliye kwenye hali ngumu
sana.
“Ehee Mungu zipokee roho zetu, na utusamee makosa yetu tuliyo yafanya. Amen”
Anna
alizungumza kwa sauti ya unyonge iliyo wafanya wezake kuendelea kulia
kwa uchungu, kwani hakuna aliye tarajia kwamba maisha yake yatakuwa
hivyo. Maneno ya Anna, yakamfanya bwana Rusev, kumwagikwa na chozi
lililo washangaza askari wake waliopo nje wakiwatazama.
Bwana
Rusev akawamrisha askari wake kuingia ndani na kuwechukua Fetty na
wezake, ambapo akawaamrisha wavalinye vipande vya vigunia vyuesi kwenye
vichwa vyao wasijue ni wapi wanapelekwa.
Wakatolewa
ndani ya chumba hicho huku wakiwa wamebebwa, kwenye mabega ya askari
walio jazia miili yao kwa mazoezi magumu wanayo yafanya kila kukicha.
Moja kwa moja wakawatoa nje ya jumba hilo na kuwaingiza kwenye helcoptar
ambapo bwana Rusev naye akaingia ndani ya helcoptar hiyo. Mtiani mkubwa
kwa Fetty na wezake ni kujua ni wapi wanapo kwenda, kutokana hawakuwa
na jinsi yakufanya huku mikono yao ikiwa imefungwa pingu na miguu yao
ikiwa imefungwa minyororo mirefe.
Mwendo
wa lisaa zima wakawa wapo angani, ambapo moja kwa moja wakafika
katikati ya kina cha bahari, ambapo helcoptar hiyo taratibu ikaanza
kushuka chini. Kutokana haoni chochote ikawa ni ngumu kujua ni kitu gani
kinacho fwata mbeleni. Jinsi helecoptar hiyo, ilivyo zidi kushuka chini
ndivyo sehemu hiyo kubwa ya maji ilivyo anza kujigawa. Maji ya sehemu
kubwa yakatawanyika na mfuniko mkubwa wa chuma ukafunguka na kuiruhusu
helcoptar hiyo kuingia ndani, ambapo ndipo kuna kambi kubwa ya silaha ya
bwana Rusev, ambayo si rahisi kwa mtu kuweza kugundua swala hilo.
Kutona
na utaalamu mkubwa waliweza kujenga ngome kubwa chini ya bahari ambapo,
ipo ndani ya miamba. Ambapo wameweza kutengeneza hewa ya oksijeni,
wanayo weza kuitumi ndani ya miamba hiyo mikubwa huku taa kubwa za umeme
zikiwa zinawaka masaa 24.
Wanajeshi
wote wanao ishi kwenye ngome hiyo ni makomandoo na niwatu wenye vipaji
maalimu, ambao bwana Rusev aliweza kuwachukua sehemu mbalimbali dunia,
na kuwaweka pamoja na kuanza kutengeneza silaha ambazo ni adimu sana
duniani. Huku siku hadi siku wakitengeneza mabomu ya nyuklia, ambayo ni
hatari pale yanapo tumiwa kwenye kushambulia sehemu yoyote kwenye
kiumbe, hai nilazima kitaatjirika vibaya.
Fetty
na wezake wakapokelewa na wanajeshi, wakapelekwa kwenye wodi, kabla
hawajatolewa vipande vya magunia kwenye vichwa vyao, wakachomwa sindano
za usingizi, ambazo zikawafanya wapoteze fahamu na kulala fofofo.
Wakaanza kuhudimiwa kwenye majeraha yao yote pasipo wao kujigundua.
“Mkuu hawa ni kina nani?”
Daktari mmoja aliuliza kwa lugha ya kirusi.
“Hawa mabinti wananifaa sana kwenye kazi yangu, hakikisheni afya zoa zinatengemaa na kuwa katika hali nzuri sawa”
“Sawa mkuu”
Bwana
Rusev akatoka kwenye wodi walipo lazwa Fetty na wezake kisha na kwenda
kufwatilia utendaji wa kazi wa vijana wake ndani ya ngome yake hiyo.
***
Taratibu
vimistari vya mashine, iliyopo pembei mwa kitanda alicho lazwa Rahab,
ikaanza kuonekana vikiwa vimepinda pinda, ikiashiria kwamba ameanza
kupumua hii ni baada ya madaktari kuendelea kuustua moyo wake kwa
kutumia mashine maalumu za kuweza kustulia mapigo ya moyo. Ikawapa
nafasi madakari kuweza kufanya uchunguzi wa kina juu ya tatizo lililo
mkumbwa Rahab.
Raisi
Praygod akazidi kumuomba Mungu, huku macho yake akiwa ameyatoa kwenye
mashine iliyo endelea kuonyesha vimistari vidogo vya kijani ikiashiria
kwamba mke wake ameanza kupumua. Baada ya kusimama kwa muda mrefu,
Fredando akamchukua raisi Praygod hadi kwenye moja chumba cha mapumziko,
ambacho mara nyingi hukitumia pale anapokuwa anazungumza na madaktari
wake.
Matokeo
ya majibu ya vipimo, ikawa ni jambo la kustaajabisha kwa madaktari
ambao wakaanza kujiuliza ni nani ambaye amehusika na ugonjwa wa rahabu
“Wewe umezoeana na baso, peleka majibu”
Mmoja wa madaktari alipendekeza daktari Canter, mwanamama mpole na mchishi kuweza kupelea majibu hayo
“Hivi jamani, ni kweli haya majibu yapo sahihi”
“Jamani si sote hapa tumepima na majibu kuwa hivyo, na tukarudia kwa kipomo kingine majibi yamekuja hay ohayo”
“Wewe peleka sisi huku tuendeleaa kumugudumia mgonjwa”
Bi
canter akatoka kwenye chumba alipo lazwa Rahab, moja kwa moja akaelekea
kwenye chumba mara nyingu hukitumia kuzungumza na bosi wao. Baada ya
kuingia ndani ya chumba hicho raisi Praygod, akanyanyuka kwenye kiti
alicho kaa, na kumpokea daktati huyo kwa macho makali yaliyo jaa
wasiwasi. Frednando akamuomba daktari kukaa kwenye kiti cha pembeni
“Mke wangu anatatizo gani dokta?”
“Kaa chini kaka”
Frednando alizungumza huku akimshika mkono raisi Praygod na kumkalisha kwenye kiti alichokua amekikalia
“Tumeweza kumfanyia mgonjwa uchunguzi wa kina, na tumeweza kugundua kwamba……”
Baada
ya kfika sehemu ya tatizo linalo msumbu Rahab, dokta Canter akanyamaza
na kuwatazama matajiri wake hao, ambao wote wamemtumbulia mimacho
“Mke wako muheshimiwa, tumemkuta na….. na sumu nyingi”
“SUMUU…..!!!”
Raisi Praygod alizungumza huku akiwa anashangaa swala hilo
“Ndio sumu ambayo inaoenekana iliwekwa kwenye kinywaji alicho kunywa dakika chache kabla ya kuanza kufanya kazi mwilini mwake”
SHE IS MY WIFE(36)
Raisi
Praygod akamgeukia rafiki yake kipenzi Frednando, na kumtazama kwa
macho makali ambayo alianza kumtilia mashaka rafiki yake huyo, ila
Frednando naye alionekana kuwa hatambui lolote lililo jitokeza katika
hili swala kwani muda mwingi walikuwa pamoja.
“Ila tunaendelea kuitoa sumu iliyo ingia mwilini mwake”
“Sawa”
Frednando
alimjibu dokta Canter na kumfanya dokta huyo kuomba kunyanyuka na
kuondoka ndani ya chumba hicho huku akiwaacha Raisi Praygod na Frednando
wakiwa na maswali mengi juu ya nani ni aliye weka sumu kwenye kinywaji
cha Rahab.
**(MASAA MACHACHE KABLA)**
Kila alipo yatupa macho yake usoni mwa raisi Ptagod Makuya na mke wake
Rahab, roho ikazidi kumuuma Mercy, binti mrembo, ila ni mfanyakazi
hodari wa kupika katika jumba hili la tajiri Frednando, tangu siku ya
kwanza kumuona Praygod kuingia katika jumba hili moyo wake ulipata
shinikizo kubwa la maumivu yaliyo changanyikana na upendo mkubwa. Japo
asili yake ni mmexco halisi, ila alijikuta akimpenda mwanaume mwenye
ngozi nyeusi kama Praygod.
Halikuwa
ni jambo rahisi kuweza kulitamka swala la kumpenda Praygod kwa mtu
yoyote ndani ya jumba hili kwani alihisi kwamba itakuw ni hatari kubwa
sana kwake, kwani akilini mwake alisha anza kufikiria jambo ambalo
lingemfanya akiuke maadili ya kazi yake pamoja na sheria za nchi yake.
Ila hakuwa na jinsi zaidi ya kupanga mipango mizito kichwani mwake ya
kumuondoa duniani Rahab, ili we rahisi kwake kujiweka karibu na Raisi
Praygod, anaye onekana kudatishwa na penzi la Rahab.
Macho
ya Mercy, yaliendelea kuwashuhudia Rahab na Praygod jinsi wanavyo
endelea kufurahi wakiwa katika mavazi yakuependeza, ikiashiria kwamba
kwa sasa ni mke na mume.
Japo
ni wafanyakazi wengi wakiume waliendelea kumtamani Mercy ila hapakuwa
na aliye ambulia hata kupewa matumaini ya kuoenyeshwa kwamba amependwa
na binti huyo. Kila mmoja alijikuuta akijibiwa mbona na binti huyo
mrefu, mwenye nywele ndefu zinazo fika mgongoni, huku akiwa na umbo
fulani jembamba la kimisi, ila lenye mvuto kwani liliweza kuchukua vazi
lolote litakalo mpendeza.
Macho
ya Mercy hayakucheza mbali na Rahab, aliye shika kinywaji chake
mkononi, huku pembeni yake kukiwa na mumewe aliye endelea kuachia
tabasamu pana lililo mfanya azidi kuwa mzuri na kumchanganya Mercy.
“Oooh Mungu wangu nisaidie mimi”
Mercy
alizungumza huku mkoni mwake akiwa ameshika kitambaa alicho saga,
kidonge komoja cha sumu, kali sana inayo tumika katika kunyunyizia
katika mimea ya matunda aina ya apple, ambalo ni zao kubwa sana linalo
patikana katika nchi ya Mexco. Mercy akaanza kutafuta uwezekana na
kuweza kumuwekea unga huo Rahab kwenye kinywaji alicho kishika kwenye
mkono wake. Wakati wa kuwasalimia maharushi na kuwapa mikono ikawa ndio
nafasi ya pekee kwa Mercy kuweza kutimiza adhima yake kwa Rahab.
Wakatu
wakaanza kupita walio maharusi, huku wengine wakiwakumbatia maharusi
kwa ishara ya kuwapongeza. Mercy akaanza kumkumbatia raisi Praygod huku
kwenye vidole vyake akiwa ameshika chenhachenga kidogo za unga wa sumu,
alipo mfikia Rahab, akamkumbatia na kupata nafasi ya kunyunyiza unga wa
sumu kwenye kinywaji cha Rahab pasipo mtu yoyote kuweza kushuhudia tukio
hilo, akampiga mabusu kadhaa Rahab ya mashavuni, huku moyoni mwake
akiwa akiwa na furaha kwani Rahab kwa muda wowote anaweza kuja na kuwa
marehemu mtarajiwa.
Kitu
kilicho anza kumshangaza Mercy ni jinsi Rahab alivyo anza kupata ugumu
wa kunywa kinywaji hicho, kwa mara kadhaa Rahab alikipeleka kinywaji
hicho hadi mdomoni mwake ila akakirudisha na kujikuta akizungumza au
akitabasamu na memewe aliye onekena kujawa na furaha sana.
“Foolish”(Pumbavu)
Mercy
alizungumza baada ya kusikia kwamba bosi wao amewakabidhi ndege ya
kifahari Raisi Praygod pamoja na Rahab. Akawashuhudia Rahab, Praygod na
Frednando wakielekea kwenye ndege na kuingia. Mercy akaondoka kwa hasira
eneo la sherehe na kuelekea chumbani kwake, akajifungia na kujirusha
kitandani mwake na kuanza kupiga piga mto wake kwa ngumi, kwani ni
maumivu mazito ya mapenzi yaliuchoma mayo wake hadi jasho jembamba
likaanza kumwagika.
Ndani
ya nusu saa akaanza kusikia ving’ora vya gari la wagonjwa, kwa haraka
akakimbilia dirishani na kufungua kutazama nje, kutokana na chumba chake
kuwa gorofa ya nne kwenda juu, aliweza kushuhudia jinsi madaktari wao
wakifanya juhudi za kumpa huduma ya kwanza Rahab, mara baada ya
kumshusha kwenye ndege.
“I win”(Nimeshinda)
Alizungumza
huku tabasamu akiendelea kuliachia, sasa akilini mwake akatambua kwamba
kinacho fwata hapa ni yeye kuanza kujiweka karibu na Praygod kwani
amefanikiwa kumuondoa adui yake namba moja, japo Rahab hakuwahi
kumfanyia jambo lolote ambalo alipaswa kumlipizia kisasi kwa
kumsababishia kifo.
***
Frednando akamuaga Rais Praygod, akatoka nje ya jengo la hospitali huku
moyoni mwake akiwa amefadhahika sana kwa kile kilicho tokea kwa mke wa
rafiki yake kipenzi Praygod.
Akaingia
kwenye gari lake na kumuamrisha dereva aendeshe kwa kasi gari hilo hadi
nyumbani kwake, huku akipiga simu kwa msimamizi mkuu wa jumba lake
aweze kuandaa kikao kikubwa na wafanyakazi wote walio hudhuria kwenye
sherehe ya harusi muda mchache ulio pita.
Ndani
ya dakika kumi akawa amefika kwenye jumba analo ishi, kuingia sebleni
akawakuta wafanyakazi wake wote wakiwa kwenye mkao wa kumsubiria bosi
wao huyo, ambaye huwa mara nyingi hapendi ujinga na swala la kumuondoa
mtu duniani kwa kumtandika risasi ni dogo sana kwake, endapo mtu huyo
ataonekana kuenenda kinyume na taratibu zake alizo ziweka kwa
wafanyakazi wake hao.
Frednando
akapita katikati yao huku akioenekana kukasirika hadi rangi ya ngozi
yake kubadilika na kutawaliwa na uwekundu fulani. Akawatazama
wafanyakazi wake karibia wote kutokana na wingi wao, hakuweza kuzitazama
sura zote.
“Esto es ridiculo”(Huu ni ujinga)
Frednando
alizungumza kwa lugha ya kispain, huku akiwfoka kwa sauti ya juu, na
kuzidi kuwaogopesha wafanya kazi wake hao, ambao wengi humuogopa sana
bosi wao.
“Quien habĺa puesto veneno en ;a bebida de Rahab”(Ni nani aliye weka sumu kwenye kinywaji cha Rahab?)
Ukali
was suati ya Frednando, ikapenya masikioni mwa Mercy aliyekuwa akishuka
ngazi kuja chini sebleni kusikiliza kikao walicho itiwa na bosi wao
huyo. Ikambidi asimame kuchungulia chini na kuona wezake wakiwa
wamesimama kwenye kundi kubwa hku kila mmoja akionekana kuwa makini na
kumsikiliza bosi wao
“Jefe
habria sido mejoe si vemos los videos gue se graban en toda la boda sel
acontencimento”(Bosi itakuwa ni vizuri tukitazama viseo zilizo
rekodiwakwenye tukio zima la arusi)
Mshauri
wa Frednando alitoa wazo ambalo kila mmoja alionekana akingong’ona
akiamini hiyo itakuwa ni njia mafaka kwa wao kuweza kumjua ni nani
muhusika. Wazo hilo likamfanya Mercy kuanza kutetemeka mwili mzima na
kushindwa kushuka chini zaidi ya kujibanza kwewye sehemu alipo simama na
kuendelea kutazama ni nini kitakacho fwata.
Mafundi
mitambo walio husika na swala zima la kurekodi matukio yaliyo tokea
kwenye harusi, wakaunganisha picha za matukio yote kwenye mkanda mmoja
kisha na kuuweka kwenye kifaa maalumu cha kuwezesha mkanda huo kuonyesha
katika tambaa kubwa lililopo sebleni, taa zote zikazima na kubakiwa na
mwanga wa mkali wa kifaa kilicho kuwa kinamulika kwenye tambaa hilo na
kuonyesha matukio yoyote.
Mercy
naye hakuwa mbali katika kutupia macho yake kwenye video hiyo inayo
onekana na wezake wote pamoja kwenye seble hiyo kubwa. Ikafika wakati
wakiwapa mikono maharusi kwa ishara ya kuwapongeza. Mercy akajiona
akipita kwa Raisi Praygod kisha akafika kwa Rahab na kumkumbatia huku
akipimpiga mabusu.
“Detener inmediatemente”(Simamisha hapo hapo)
Frednando
alizungumza kwa sauti ya juu na kumfanya muongozaji wa video hiyo
kusimamisha sehemu inayo muoenyesha Mercy akimkumbatia Rahab kwa furaha.
Mercy akajikuta akiitumbualia macho sehemu hiyo iliyo simamishwa huku
mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana.
No comments:
Post a Comment