Advertisement

Breaking

Tuesday, August 30, 2016

Mtoto wa Shule Alivyofumaniwa na Mwanaume wa zaidi ya Miaka 60 Tanga

August 29 2016 Kupitia Hekaheka ya Clouds FM Geah Habib ametuletea Hekaheka iliyotokea Tanga ambapo mzee mmoja kafumaniwa na mkewe akiwa na mtoto wa shule wa miaka 14.

Mjomba wa mtoto ameeleza kuwa mtoto amekuwa akijiandaa asubuhi na mapema sana na anaaga anaenda shule lakini anapitia kwa huyo mzee na baadaye muda wa saa moja anaena shule……

Mahusiano yameanza tangia January, mpaka sasa hivi ni mwezi wa nane na sisi mpaka tumekuja kugundua ni baada ya kutokea ugomvi, mke wake yule mzee amempiga na kumng’ata mtoto ameumia na sisi ndio tukajua hilo suala.

Mtoto wangu ana miaka kumi nne na mzee huyo ana kama 60 mpaka 70 maana ni babu kabisa, sisi halikuwa hatujui tulikuwa tunajua anaenda shule na alikuwa anamuaga bibi yake maana anakaa na bibi yake kwamba wanatakiwa kuwahi namba kumbe asubuhi anaanza kwanza kwa huyo baba.

Jumatano asubuhi walipokutana na huyo baba kupewa hela mara mke wa huyo baba akatoa akaanza kumshambulia na kumng’ata

No comments:

Post a Comment

Sponsor