Advertisement

Breaking

Wednesday, August 31, 2016

Shamsa Ford Aamua Kuwaomba Msamaha Wote Aliowakosea kabla ya Harusi yake

Zikiwa zimepita siku chache tu toka habari za Shamsa Ford kutarajia kuolewa na mfanyabiashara Chid Mapenzi kuzagaa mitandaoni , Leo asubuhi kaamua kuwaomba msamaha wale wote aliyowakosea ili aweze kuanza ukurasa mpya bila kinyongo.. 

Soma hapa alichosema:

"SIKU zote tunamuomba Mwenyezi Mungu atusamehe dhambi zetu lakini sisi binadamu tunashindwa kusameana hali ya kwamba hakuna mwanadamu aliyekamilika kama MALAIKA. .Naomba nitumie nafasi hii kumuomba msamaha kila niliyemkosea katika maisha yangu iwe makusudi au kwa bahati mbaya .Naomba utafute nafasi ndani ya moyo wako kunisamehe kwasababu nahitaji kuanza ukrasa mpya wa maisha yangu bila kinyongo na mtu yeyote. .NA ww pia uliyenikosea kwa chochote nataka ujue nimekusamehe kutoka ndani ya moyo wangu. .Mungu atufanyie wepesi wa kila jambo na inshaaallah atupe nafsi za kusameana pale tunapokoseana kwasababu duniani tunapita. ...NAWAPENDA WOTE"

No comments:

Post a Comment

Sponsor