Msanii wa muziki wa hip
hop kutoka Tip Top Connection, Dogo Janja ametangaza rasmi kuwa ana mpango wa
kuoa hivi karibuni.
Rapper huyo anayefanya
vizuri na wimbo ‘Kidebe’ amesema amempata mtu sahihi ambaye anaweza kufunga
naye ndoa nakuachana na ukapera.
“Yah ni kweli nataka kuoa muda si mrefu nitavuta jiko hivyo siwezi kusema ni lini ila suala hilo lipo kwenye mchakato” Dogo Janja alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio.
“Yah ni kweli nataka kuoa muda si mrefu nitavuta jiko hivyo siwezi kusema ni lini ila suala hilo lipo kwenye mchakato” Dogo Janja alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio.
Kwa upande wa Madee ambaye
ni mlezi wa Dogo Janja kimuziki na katika maisha ya kila siku alisema kuwa
kitendo cha Dogo Janja kutaka kuoa kabla yake itakuwa kama dharau hivyo
anapaswa kusikilizia kwanza mpaka yeye afanye mambo kwanza ndipo na yeye
atangaze.
“Ha ha ha ha Dogo Janja kuoa kabla yangu itakuwa kama dharau aiseee anapaswa kusubiri kwanza mimi nifanikishe jambo hilo ndiyo yeye afuate” alisema Madee
“Ha ha ha ha Dogo Janja kuoa kabla yangu itakuwa kama dharau aiseee anapaswa kusubiri kwanza mimi nifanikishe jambo hilo ndiyo yeye afuate” alisema Madee
No comments:
Post a Comment