Advertisement

Breaking

Tuesday, October 4, 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 19 & 20

MUANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA


ILIPOISHIA...
“NDUGU ABIRIA, NIFURAHA YANGU KUWA NANYI KATIKA SAFARI HII, NIMETOA LISAA MOJA KWA KILA ABIRIA KUSALI SALA YAKE YA MWISHO KWANI NDEGE INAKWENDA KULIPUKA NDANI YA LISAA HILO KUTIMIA KAMA HUAMINI, TIZAMA HII”

Samson akaishika camera na kuigeuzia kwenye computer aliyo iietega mwendo kasi wa saa, unao onyesha dakika zake zikirudi nyuma, kwani ikifika ndani ya muda alio upanga, mfumo mzima wa ndege unakwenda kuzima, na litakalo tokea hapo ni ndege kulipuka, jambo lililo anza kumuogopesha kila mmoja aliyomo ndani ya ndege hadi raisi mwenyewe

ENDELEA...

Samson akaigeuzia kamera alipo na kuznedelea kuzungumza kwa sauti iliyo jaa msisitizo 
“NAJUA MUTASHANGAA, ILA NI KWAMBA NITAHITAJI RAISI KUFANYA HAYA YOTE AMBAYO NITAMUAGIZA KUFANYA LA SIVYO PUUUUUUU, SOTE TUTAKUFA HAHAHAAAAA”
Samson akaanza kucheka kicheko kilicho muacha mdomo wazi Rahab ambaye hadi sasa hivi amuelewi Samson anamalengo gani na roho yake

Fetty, Anna, Agnes na Halima hawatambui ni wapi wanapo elekea, kila mmoja akabaki akiwa na wasiwasi moyoni mwake kwani, nyuso zao bado zimefunikwa na vitu mifuko mnyeusi, isiyo wapa uwezi wa kuona kinacho endelea zaidi ya pumzi zinazo ingia kwenye pua zao.Kila mmoja anahofu ya kuuliza ni wapi wanakwenda kutokana kila jibu walilo pewa apo awali ni kwamba wanaelekea kuzimu.Wakasikia mlango wa chuma ukifunguliwa kwenye chumba walichopo.
“Yupi mkuu”

Sauti ya mwanaume ilisikika kwenye masikio yao, na hawakujua ni nani anaye uliziwa
“Huyu mwenye mahipsi makubwa” 
Mkuu wa askari alijibu kupitia redia ya upepo, huku akitazama kwenye moja ya Tv iiyopo kwenye chumba chake, ikionyesha video za kamera za ulinzi zilizopo kwenye chumba walichopo Fetty na wezake

“Ahaa sawa mkuu”
Askari aliye agizwa na mkuu wake wa kikosi, akamkamata Anna, na kumnyanyua juu
“Jamani munanipeleka wapi?”
Anna alizungumza huku akijitahidi kujitoa mikononi mwa askari huyo
“Tulia wewe, nitakuua malaya mkubwa wewe”
Askari huyo akamnyanyua Anna na kumuweka begani mwake, na kutoka kwenye chumba na kuuamiza mlango kwa nguvu
“Hakikisheni hatoki mtu hapa”

Askari huyo aliwaagiza askari wengine wawili, walio simama kwenye malango wakilinda chumba walichopo majambazi hawa wa kike.Askari aakendelea kumbeba Anna ambaye anaendelea kufurukuta kwenye bega lake alipo muweka, kutokana na ukubwa wa misuli yake iliyo jengeka vizuri kutokana na mazoezi ya kijeshi anayo yafanya, Anna hakumsumbua kabisa kuchomoka kwenye mikono yake.Wakafika kwenye moja ya chumba ambacho yupo mkuu wake wa kikosi bwana Mathiasi Reymond na kumuingiza Anna na kumkalisha kwenye kiti
“Tulia kama ulivyo la sivyo tutakunyonga”

Anna aliendelea kupokea vitisho kutoka kwa askari aliye mtoa kwenye chumba alicho kuwepo na wezake.Mathiasi Reymond, tayari amesha vua ngua zake na kubaki na bukta yake ya ndani kwa ajili ya kufanya kazi moja tu, yakumuingilia kimwili Anna, msichana mzuri aliye umbika kila idara ya mwili wake.

Fetty akanyanyuka kwenye kwenye sehemu aliyo kaa, lengo lake ni kusikiliza kama atapokea amri yoyote ya kuambiwa kukaa kwenye sehemu yake, ila ukimya ukatawala.Akapiga hatua za taratibu akizunguka kwenye chumba akijaribu kujua ni kitu gani kinacho endela ila hakusikia chochote.

“Jamani mupo”
Fetty alizungumza kwa sauti ya chini
“Ndio, ila tupo wa tatu”
Halima alijibu kwa sauti ya kunong’oneza
“Nalijua hilo, Anna atakuwa amepelekwa wapi?”
“Yaani hata mimi mwenyewe sielewi?” Agnes alijibu
“Sijui hapa ni wapi jamani” Agens aliiuliza
“Cha msingi ni kujua nini tunatakiwa kukifanya na amini mumenielewa”

Fetty alizungumza huku akijiegemeza kwenye ukuta wa chumba alichopo, kutokana na mikono yake kufungwa kwa nyuma kwa pingu na kugundua si ukuta wa kawaida

Mathiasi Reymond akamuamuru mlizi wake, kumfungua  vipingu za mikononi na minyororo aliyo fungwa Anna kwenye miguu yake na mlinzi wake akafanya kama alivyo agizwa na bosi wake.Baada ya mlinzi wake kumfungua Anna akatoka ndani ya chamba na kumuacha bosi wake na Anna
                                                                                              
Vichwa vya viongozi wa pande zote mbili Tanzania na Marekani vinazidi kuuma, kila mmoja akijaribu kutafuta mbinu na njia za kuweza kuipata ndege yenye thamanini sana aina ya Air Force inayomilikiwa na serikali ya nchini Tanzania huku ndani mwake ikiwa imembeba raisi pamoja na viongozi wapambe wake.Juhudi za Satelait katika kuinasa ndege ya raisi na kutambua ni wapi ilipo inafua dafu, jambo linalo zidi kuwachanganya sana viongozi wa pende zote mbili.

Wanacho kihofia viongozi wa nchini Tanzania ni kumpoteza raisi wao mpendwa bwana Praygod Makuya, huku serikali ya Marekani ikihofia kupoteza moja ya ndege zake ambazo ina uwezo mkubwa wa kuhimili mikiki mikiki ya vita ya anga japo imetengenezwa kistarehe zaidi kwa ajili ya kumbeba raisi huyu wa Tanzania aliye jijengea umaarufu mkubwa sana kutokana na ucheshi wake na ushirikiano wake kwa wananchi na vingozi mbali mbali duniani, katika mataifa tajiri na mataifa masikini

“Inatuazimu kutumia, mpango namba mbili(Plan B)”
Mkuu wa jeshi la anga alizungumza na mkuu wa jeshi la anga nchini Tanzania kwa kupitia mtandao wa kuonana moja kwa moja katika vioo vya Tv zao kubwa zilizopo kwenye maofisi yao ya jeshi.

“Njia gani?”
“Nimezungumza na raisi wangu, amenipa ruhusa ya kutuma ndege zangu za kijeshi kufwatilia mzunguko mzima wa ndege ya raisi ilipo pitia”
“Asante sana, nitashukuru kama ukifanya hivyo”
“Sawam na pia nitahakikisha kwamba, hakuna kitu kitakacho kwenda kinyume na mpango, na kama itakuwa ipo chini ya watekaji, kikubwa ni kumuokoa raisi tu”
“Sawa”
  
“MOJA, NINAHITAJI RAISI, KUJA KATIKA CHUMBA CHA MAWASILIANO, AKIWA PEKE YAKE NA PASIPO KUWA NA SILAHA YA AINA YOYOTE”
“MBILI…..OOOHH NITAZUNGUMZA BAADAYE, MUHESHIMIWA RAISI NINAKUPA DAKIKA TATU KUANZI SASA HIVI, NA NINAKUONA HAPO ULIPO NA USIJARIBU KUFANYA UJINGA WOWOTE LA SIVYO UTAANGAMIA”
Samson akazima kamera yake na kumtazama Rahab ambaye muda wote Samson alipokuwa akizungumza yeye alikuwa yupo kimya

“Hilo ni bomu?”
Rahab aliuliza huku sura yake kwa mbali ikionyesha wasiwasi wa kuangamia, Samason akamtazama kwa muda Rahab jinsi anavyo hema japo anajaribu kujikaza

“Kwa nini una wasiwasi?”
“Nimekuuliza tu, ila sina wasiwasi”
“Ndio ni bumu, unaogopa kufa”
Samson alizungumza huku akimsogelea taratibu Rahab, kisha akamshika Rabab kidevu na kutazamana naye kwa sekunde kadhaa kisha akaanza kuinyonya midomo ya rahab taratibu

“Nakupenda Rahab wangu”
Samson alizungumza kwa sauti iliyo jaa mahaba, ila Rahab kichwani mwake akaanza kupanga mpango tofauti na Samson, kwani hadi sasa hivi aelewi  ni kitu gani anacho kifikiria Samson kwenye mpango waliio upanga

Kwa utaratibu mkubwa, huku akishusha pumzi zake, bwana Mathiasi Reymond akaanza kumpapasa Anna mapaja yake, huku kila mara akimeza mafumba ya mate, akazidi kuipandisha mikono yake taratibu hadi kwenye kiono cha Anna na kuendelea kukitomasa, jambo lililo anza kumoa wasiwasi mwingi Anna.Akaendelea kuipandisha mikono yake hadi kifuani mwa Anna na kuzidi kumtomasa kwa nguvu Anna kwenye maziwa yake.Mathiasi Reymond, akamvua fuko jeusi alilo vishwa Anna kichwani na kukutana na sura ya binti mrembo, ambaye ukiambiwa kwamba ni jambazi tena hatari ni lazima ukatae tena kwa nguvu zote

Macho ya Anna yakazidi kulishangaa jitu kubwa. Lenye tumbo kubwa lililo shikana na mijiziwa mikubwa inayo ning’inia mithili ya kifua cha mama anaye nyonyesha, rangi yake ya mwili ikiwa ni nyeusi ikikimbizana na mkaa ulio pauka.Mihemo ya bwana Mathiasi Reymond, inazidi kumchefua Anna ambaye tayari bwana Mathiasi amesha mfungua, vifungo vya nguo lake alilo valishwa
“Wewe ni mzuri sana”

Bwana Mathiasi alizungumza huku mikono yake akiipeleka kichwani mwa Anna, na kwakutumia nguvu zake zote akaivuta shingo ya Anna karibu yake, na kuanza kumng’anganiza kuikutanisha midomo yao.Kutokana na uchovu na kuzidiwa nguvu na Bwana Mathiasi Reymond, Anna akajikuta midomo yake ikitua kwenye midomo ya Bwana Mathiasi na kiasi cha mate ya bwana Mathiasi kikiaanza kuingia kinywani mwake.Anna taratibu akaanza kujilegeza, na kumfanya bwana Mathiasi kupunguza kiasi kikubwa cha nguvu anazo zitumia.

Gafla Anna kwa nguvu zake zote alizo jaliwa na Mungu, akaing’ata midomo ya chini ya bwana Mathias Reynmond, na kujikuta akipokea ngumi nzoto, iliyo tua tumboni mwake na kumlegeza mwili...

             SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……20

....Mathis Reymod akamnyanyua Anna na kumtupia kitandani, kwa kutumia minguvu yake mingi akalichana vazi alilovaa Anna
“Tulia wewe”
Mathis alizungumza huku akihema sana mithili ya bata mzinga aliye kimbia kwa umbali mrefu, akaendela kuyachezea maziwa ya Anna ambaye muda wote anajitahidi kuulinda utu wake kama mwanamke anaye jiheshimu mbele ya mwanaume asiye mpenzi wake.Kibao kikali kikatua shavuni mwa Anna na kumfanya atokwe na kiasi cha damu kadhaa kwenye mdomo wake, hii ni baada ya meno yake kuung’ata ulimi wake kwa bahati mbaya baada ya kutandikwa kibao na Mathia Reymond.Anna akaanza kujilegeza huku nguvu za mwili wake zikianza kumuishia taratibu, akajikuta akimuacha bwana Mathias kufanya anacho jisikia kufanya katika mwili wake.

Kwa bahati mbaya ama nzuri kwa Anna, uume wa Bwana Mathias Reymond, hajaweza kusimama kama kawaida yake, jambo ambalo likaanza kufedhehesha bwana Mathias, kila mbinu aliitumia ila kuusimamisha mpigo wake, haikuwezekana na kujikuta jasho jingi likimwagika, huku macho ya uchu yakiwa yametua kwenye mwili wa Anna, ambao hauna nguo hata moja.

Anna akayanyua macho yake kwa uchovu mwingi, huku yakiwa yamejawa na ukungu wa machozi yaliyokuwa yakimwagika kimya kimya, akamkuta bwana Mathias Reymond akiendelea kuuchua mpingo wake, ambao hadi sasa hivi umeelekea chini, ukikataa kabisa kufanya shuhuli aliyo ikusudia kuifanya kwa binti mrembo Anna
“Ni ingize sasa”

Anna alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, sauti yake ya uchungu ikazidi kuusisimua mwili wa bwana Mathias Reymond na kujikuta akitoka kwenye umakini wa kuzifuta hisia zake ili kuusimamisha mpingo wake.Anna akanyanyuka na kumlaza kitandani bwana Mathias Reymond, kisha akamkalia kwenye kiuno chake
“Wewe si unataka kunifanya, nifanye sasa”

Anna alizidi kumtia uchungu bwana Matias ambaye hadi sasa hivi, mapigo yake ya moyo yanakwenda kasi huku jasho jingi likimwagika.Anna akaanza kazi ya kumkomoa bwana Mathias, akaushika mpingo wa bwana Mathias Reymond na kuanza kuuchezea tararibu, ila haukufanya kazi, 

“Nyanyuka na ukae”
Anna alizungumza na bwana Mathias Reymond akatii, Anna akamkalia bwana Mathias kwenye mapaja kisha akaipitisha miguu yake na kukutana mgongoni mwa bwana Mathias Reymod
“Unanipenda?”
“Ndio”

Mathias alijibu huku wasiwasi mwingi ukiendelea kumsumbua, na mawazoni mwake akijikuta akijutia ni kwanini alimchukua mwanamke huyu kwani, ni moyo ya aibu kubwa ambayo ameipata mbele ya binti mbichi kiasi hichi, isitoshe na hii ndio mara yake ya kwanza kukutana na binti huyu na mbaya zaidi alitumia nguvu nyingi sana, ila ndio hivyo hadi sasa hivi hajaweza kufaidika na chochote.

Anna akaanza kuinyonya midomo ya bwana Mathias Reymond na kuzidi kumchanganya, kwa kutumia nguvu zake zote za minguu, Anna akaanza kuzibana mbavu za bwana Mathias Reymond, na kumfanya anza kuhisi maumivu.Anna akaendelea kufanya zoezi lake la kazibana mbavu za bwana Mathis Reymond, huku mdomo wake ukiendela kuirudisha pumnzi ya bwana Mathias ndani, ambayo anajaribu kuitoa kwa wingi kupitia mdomo wake
“Uu..naaniu……aaaa”

Bwana Mathias Thomas alizungumza kwa shida nyingi sana, huku machozi yakianza kuwamwagika, akili na mawazo yake yote ameyapelekea kwamba ni miongoni mwa mchezo wa kitandani, utakao msaidia kuufanya mpingo wake kusimama na kufaidi tunda la Anna.Ila sivyo kama anavyo wazia kwani Anna, akilini mwake anawaza kumuangamiza bwana Mathias kwa mfumo huu alio uchagua, wa kumuua kimya kimya.Bwana Matias akaanza kutoa sauti iliyo jaa mikwaruzo, huku macho yake yakiwa yamemtoka  mithili ya mtu anaye karibia kukata roho.

Anna akazidi kuongeza juhudi ya kuendela kuzibana mbavu za Mathias hadi akasikia mlio wa kuvunjika kwa mbavu za bwana Mathias Thomas, ndipo alipo chukua uamuzi wa haraka wa kuivunja shingo ya bwana Mathis Thomas na kumsababishia kifo cha kimya kimya bila mtu yoyote kusikia

“Ahaaaaa”
Anna alihema huku akijilaza pembeni ya kitanda, mwili wake wote ukiwa umelowana kwa jasho jingi lililotokana na shuhuli pevu aliyo ifanya

Ndege za jeshi la Kimarekani aina ya Jet, zinazo ingia marubani mmoja, zipatazo sita zikaanza kazi ya kutafuta ni wapi ilipo ndege ya raisi wa Tanzani bwana Pyagod Makuya ambaye hadi sasa hivi hijulikani ni wapi ilipo, marubani hao kazi yao kubwa waliyo pewa ni kumuokoa raisi huyo tu.Mwendo kasi wa ndege zao unawadaidia sana katia kulizunguka anga katika muda mchache, huku wakiendelea kuitafuta ndege ya raisi wakisaidiwa sana na satelaiti
  
Samson anamuachia Rahab na kwenda kusimama kwenye compter inayoonyesha maeneo mbalimbali ndani ya ndege ya raisi kupitia kamera za ulinzi zilizo fungwa kila sehemu ya eneo la ndege.Anaminya batani kadhaa kwenye moja ya computer na kuuruhusu mlango wa chumba ambacho yupo muheshimi Rais, kisha akaiwasha video kamera yake na kusimama kama alivyokuwa amesimama hapo awali
“Muheshimiwa raisi sasa ni muda wako kutoka, unadakika tatu kufika hapa”

Samson alizungumza kwa ufupi na kuizima video kamera yake, kisha akarudi kwenye  computer inayo onyesha picha za video.Akamuona raisi akitoka kwenye chumba alichopo na kuanza safari kuelekea kwenye chumba walipo yeye na Rahab, kisha Samson akaufunga mlango wa chumba alicho toka raisi ili kuwazuia walinzi wake kuweza kutoka nje.

“Samson, hilo bomu dakika zake si zinazidi kuyoyoma?”
“Ndio kwani vipi?”
“Mpango wetu si kulipuka na hawa watu, mpango wetu ni kumteka raisi ili wezangu wa waweze kuachiwa huru, hivi unadhani tukilipuka itakuwaje”

“Ila na wewe hukuniuliza mimi nina mpango gani katika hili”
Samson alizungumza kwa kujiamini sana
“Sikia Samson, mimi sijali kwamba una mpango gani, ila mimi ninacho kihitaji ni wezangu kuachiwa huru”
“Na mimi ninacho kihitaji ni kufa na raisi wa jamuhuri ya Tanzania.Huo ndio mpango wangu nilio nao kichwani mwangu”

“Samson zima bomu lako”
Rahab alizungumz kwa sauti ya ukali, hii ni baada ya kumuona Samson akiwa na kiburi juu ya maamuzi yake
“Sikuzote mwanamke yupo chini yangu, na utafwata kile nilicho kihitaji mimi sawa”
Samson alizungumza huku akimsogela kwa karibu sana Rahab
“Hata mimi pia ninamaamuzi yangu, na wanaume atafwata kile nilicho ninacho kihitaji mimi sawa”

Rahab alizungumza kwa kujiamini, huku sura yake akiwa aimesogeza karibu sana na sura ya Samson.Wakaendelea kutazama kwa muda, wakasikia mlango ukigongwa kwa nje na kumfanya Samason atabasamu kisha akayatupia macho yake kwenye computer inayoonyesha picha za video, akamuona raisi akiwa amesimama nje ya mlango wa chumba walichopo, akapiga hatua za kuelekea kwenye sehemu mlango unapo gongwa
“Karibu muheshimiwa Raisi”

Samson alizungumza huku bastola yake akiwa ameielekeza kwenye tumbo la muheshimiwa raisi.Akamuamuru kuingia ndani ambapo moja kwa moja akamuelekeza kukaa kwenye moja ya kiti ambacho ni chakuzunguka.Akachukua gundi kubwa lililokuwa juu ya meza iliyopo ndani ya chumba hicho, kisha akaanza kumfunga Raisi mikono yake pamoja na miguu.

“Habari yako muheshimiwa Raisi”
Samson alizungumza huku akiwa amekaa kwenye meza akimtazama Raisi Praygod Makuya kwa macho yaliyo jaa kejeli

“Ohoo nimesahau kitu kimoja muheshimiwa Raisi, bumu letu limebaki dakika kumi na nane, kabla hatujafanya puuuuuuu”
Macho ya Rahab yaliyo jaa hasira yakatua usoni mwa Samson anaye zungumza kwa dharau mbele ya Raisi

“Unanikumbuka?”
“Hapana”
“Aaahaa sasa kuna ishu moja nahitaji umsaidie huyo mke wangu hapo, anaonekana kununa sana kutokana na nyinyi kuwateka wezake”
Rahab akashusha pumzi kidogo baada ya kusikia swala la wezake likizungumzwa

“Kuna wasichana wanne ambao mumewateka, ambao ni nani vilee”
“Ni Fetty, Agnes, Anna na Halima”
Rahab alijibu huku naye akipiga hatua akielekea alipo simama raisi na Samson.
“Hao mimi ni vijana wangu na ninahitaji uweze kuwaachia huru sawaa”

“Niliapa kuitumikia nchi yangu, na kuilinda katiba ya nchi yangu siwezi kufanya jambo kama hilo katika maisha yangu”
Raisi Praygod alizungumza kwa kujiamini sana huku akimtazama Samson na Rahab, ambao baada ya kusikia jibu hilo sura zao zikaanza kujaa mikunjano huku kila mmoja akikasirishwa na jibu hilo

“Etii eheee”
Samson alizungumza kwa dharau
“Ndio, kama munaniua niueni tu, naju nitakufa kwa ajili ya nchi yangu.Ila siwezi kubadilisha mawazo juu ya hilo swala munalo lihitaji nyiniyi”

Rahab akaachia kofi zito lililo tua shavuni mwa Raisi hadi, Raisi akaanza kujihisi kizunguzungu
“Utawaachia au uwaachii?”
Rahab aliuliza kwa hasira huku bastola yake akiwa ameishika vizuri kwenye mikono yake akiielekezea kichwani mwa Raisi
“Nenda kuzimu, malaya mkubwa wewe”

Raisi alimtukana Rahab huku akimtemea mate yaliyo tua juu ya uso wa Rahab na kuzidi kumpandisha hasira zaidi.Rahab akawa kama mbogo jike aliyejeruhiwa kwa risasi, akamtandika kichwa kikali raisi, cha pua, huku akiachia ngumi nyingi zilizo tua kwenye kifua cha Raisi
“Utawaachia uwaachii?”

Rahab aliendelea kuzungumza kwa hasira, huku muda wote Samso akawa na kazi ya kufunga mitambo yake ya kamera, na kuminya moja ya computer iliyopo katika eneo hilo
“SIWATOI”
Rahab bila ya huruma akaendelea kumtembezea Raisi mkong’oto mkali, jambo lililo zidi kumfurahisha Samson
“Ohooo baby punguza jazba”

Samson alizungumza huku akimshika kwa nyuma Rahab na kumsogeza katika eneo ambalo yupo Raisi, mikono yote ya Rahab imejaa damu za Raisi Praygod, ambaye hadi sasa hivi sura yake imejaa damu nyingi, huku baadhi ya sehemu za mwili wake zikiwa zimevimba kwa kiasi kikubwa,
“Tulia baby”

Samson alizungumza kwa sauti ya upole na kumfanya Rahab kutulia, Samso tayari ameiunganisha mitambo yake moja kwa moja na chanel zote nchini Tanzania, na kuzima mitambo yote ya Tv hizo na picha inayo onekana ni picha za Camera yake.Samson akasimama mbele ya kamera yake ambayo inammulika kuanzia kifuani hadi miguuni

“NDUGU WANANCHI, TANZANIA, NINAIMANI KWAMBA HII NI ALFAJIRI TAKATIFU KWENU, NA KILA MMOJA ANAJIANDAA KWENDA KWENYE MIZUNGUKO YAKE YA KUMPATIA CHOCHOTE KITU, ILA MIMI NAMI NINAOMBA LEO NIWAPATIA CHOCHOTE KITU, ILI SIKU YENU NZIMA IPATE KUWA NJEMA NA YAKUPENDAZE”

Samson alizungumza, jambo ambalo liliwastua wananchi wengi nchini Tanzania, ambao wamefungulia Tv zao asuabuhi wakijiandaa kwenda makazidi.Kila ambaya amewasha Tv yake akawa na shauku ya kutaka kujua ni kitu gani ambacho mtu huyo anakizungumza kwa maana chaneli ambayo inaonekana muda huu, haina jina na ndio mara ya kwanza kuonekana.Kila mwenye mtambo wa Tv yake anajaribu kuitoa chanel hii inayo onekena ila anashindwaa.

“OHOO, MUSIPATE SHIDA KWA KUITOA HII CHANEL KWENYE VYOMBO VYENU VYA HABARI, KWASABABU HII INATOKA MOJA KWA MOJA ANGANI KWENYE DEGEEE KUBWAAAAA LA RAISI WENU MPENDWA PRAYGOD”
“NINATAKA MUONE MUMUONE RAISI WENUA ANAVYO FANANIA”

Samson akaishika video kamera yake na kuielekezea alipo kaa raisi Praygod Makuya, miooyo ya watu wengi ikastuka baada ya kumuona raisi wao akiwa anavuja damu nyingi usoni mwake, Viongozi wa jeshi na mawaziri wakabaki midomo wazi, kwani hawakutegemea hali ya raisi itakuwa kama wanavyo iona hivi sasa kwenye Tv yao kubwa iliyopo kwenye ofisi walishinda macho usiku kucha wakijitahidi kutafuta niwapi ilipo potelea ndege ya raisi.

“HUYO NDIO RAISI WENU, NIMEMUOMBA AWEZE KUWAACHIA WATU WANGU WALIO KAMATWA ILA KAKATAA NA MIMI SINA JINSI NIMEONA NI VYEMA RAISI NA WATU WOTE WALIOMO NDANI YA HII NDEGE TUFE KAMA HIVI”

Samson akaigeuza kwa haraka video camera yake sehemu ilipo computer yake inayo onyesha jinsi bomu linavyopunguza dakika zake kwa kasi na hadi sasa hivi zimebaki sekunde tatu ambazo Samson aliza kuzihesabu zikirudi nyuma
“TATU, MBILI, MOJA”

Mlipuko mkubwa ulio ambatana na moto ukasikika machoni masikioni na watazamaji wa Tv walio kuwa wakilifwatilia tukio zima, na Tv zao zote, ndani ya sekunde mbili zikabadilika na kuwa chenga jambo lililo waacha midomo wazi Watanzania wengine na wengine kushindwa kustamihili ujasiri na kujikuta wakiangua vilio hadharani
 ITAENDELEA...

No comments:

Post a Comment

Sponsor