Advertisement

Breaking

Wednesday, October 12, 2016

Taarifa mpya ya Mkuu wa Mkoa kuhusu tukio la kupigwa kwa Mwanafunzi Mbeya Day


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makala amesema kuwa wanafunzi wa ualimu na walimu waliohusika na tukio la kumpiga mwanafunzi katika Shule ya Sekondari ya Kutwa Mbeya tayari wanaendelea kuhojiwa na Jeshi la Polisi kufuatia tukio hilo.

Licha ya kuwa tukio lile halikuwa adhabu sahihi kwa mwanafunzi, Mkuu wa Mkoa amewataka wazazi kujijengea tabia ya kuwafuatilia watoto wao kwani ameleeza kuwa nidhamu ya wanafunzi wa shule hiyo ni mbovu sana hasa kwa wanafunzi wa kidato cha tatu na cha nne.

Mkuu wa mkoa ameeleza kuwa, kuna wakati darasa lenye wanafunzi 50, mwalimu anafundisha wanafunzi 10 pekee wengine wakiwa hawamo darasani na mara kadhaa wanapishana na mwalimu wakati wanaingia wao wanatoka.

Wanafunzi wengine wamediriki hata kukunjiana ngumi na walimu, hivyo baadhi ya walimu ili kuepusha shari wamewaacha wafanye waoonavyo vyema.

Mkuu wa mkoa amesema kuwa wataendelea kufanya uchunguzi kuwabaini wanafunzi wakarofi zaidi na adhabu stakihi zitachukua hatua mara moja ili kuweza kurejesha nidhamu katika shule mkoani humo.

No comments:

Post a Comment

Sponsor