Advertisement

Breaking

Monday, October 31, 2016

Faraja Kotta Azungumza Hili Baada ya Miss Tanzania 2016 Diana Edward Kuandamwa Mitandaoni

Aliyewahi kuwa mshindi wa Miss Tanzania kwa mwaka 2004, Faraja Kotta Nyalandu amechukizwa na yale yanayoendelea katika mitandao ya kijamii juu mshindi wa taji la Miss Tanzania 2016, Diana Edward.
faraja

Hatua hiyo imekuja baada ya watu katika mitandao ya kijamii kuanza kumshambulia mshindi huyo juu ya umri wake. Hata hivyo kamati ya Miss Tanzania ilitolea ufafanuzi juu ya suala hilo.

Miss Faraja Kotta ambaye na yeye pia alipitia kipindi kigumu pindi alipotangazwa mshindi, ameandika ujumbe huu:


"Niliposhinda Miss Tanzania, kuna mtangazaji fulani (tena wa kiume) wa kipindi cha redio cha asubuhi alitumia kama saa nzima hewani kusema ambavyo sikustahili kushinda. Asubuhi ya Jumatatu kama leo baada ya weekend ya shindano.

Nilipigiwa simu kuamshwa. Nakumbuka niliamka nikawasha redio na nikasikiliza kipindi chote, peke yangu, chumbani.
Nilitetemeka, nilishindwa kuoga, kula, nilijifungia ndani siku nzima nikilia. Niliwaza sana ambavyo pengine ni kweli sikustahili. Nilijuta kushiriki Miss Tanzania.

I was young and naive. I had just turned 19, coming straight from the safety nets of Catholic nuns boarding schools. Sikujua kuna watu wanaweza kuwa na roho mbaya hata kwa watu wasiowajua.

It took my parents (RIP) na kila busara waliyonayo kunifanya nijisikie vizuri. I had to dig deep inside me to regain my purpose. I was exposed to a cruel world and yes, I quickly learnt, it is what it is.

Leo hii hakuna binadamu mwenye hiyo nguvu niliyompa yule mtangazaji. I learnt the hard way but I am grateful for the lesson. Thank God I learnt early. Kuna sehemu ya nguvu niliyo nayo leo iliyotokana na kujeruhiwa na binadamu na kupona. Lakini si kila mtu atapata bahati ya kupona, unaweza kumjeruhi mtu na akapotea moja kwa moja. Usijitafutie laana za reja reja.
To the newly crowned Miss Tanzania, Do you honey!

To the rest of us, tujenge zaidi ya kubomoa. Love doesn’t cost a thing!
God bless,
Faraja"

No comments:

Post a Comment

Sponsor